1Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
1Nii ei ole nüüd enam mingit hukkamõistu neile, kes on Kristuses Jeesuses.
2Maana, sheria ya Roho iletayo uzima kwa kuungana na Kristo Yesu imenikomboa kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.
2Sest elu Vaimu seadus Kristuses Jeesuses on vabastanud su patu ja surma seadusest.
3Mungu ametekeleza jambo lile ambalo Sheria haikuweza kutekeleza kwa sababu ya udhaifu w binadamu. Mungu alimtuma Mwanae akiwa mwenye mwili sawa na miili yetu sisi wenye dhambi, ili aikabili dhambi, na kwa mwili huo akaiangamiza dhambi.
3Sest seda, milleks Seadus oli võimetu, kuna see oli jõuetu inimloomuse tõttu, on teinud Jumal, kes mõistis patu inimeses surma, läkitades oma Poja patuse loomuse sarnasuses ja patu pärast,
4Mungu alifanya hivyo kusudi matakwa ya haki ya Sheria yatekelezwe kikamilifu ndani yetu sisi ambao tunaishi, si kwa nguvu za kibinadamu, bali kwa nguvu ya Roho.
4et Seaduse nõuded oleksid täidetud meis, kes me ei käi oma loomuse, vaid Vaimu järgi.
5Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
5Sest need, kes elavad loomuse järgi, mõtlevad lihalikke mõtteid, kes aga Vaimu järgi, need Vaimu mõtteid.
6Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uzima na amani.
6Sest lihalik mõtteviis on surm, Vaimu mõtteviis aga elu ja rahu;
7Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
7seepärast et lihalik mõtteviis on vaen Jumala vastu, sest ta ei alistu Jumala Seadusele ega suudagi seda.
8Watu wanaotii matakwa ya mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
8Kes elavad oma loomuse järgi, need ei suuda meeldida Jumalale.
9Lakini ninyi hamuishi kufuatana na matakwa ya mwili, bali kufuatana na matakwa ya Roho, ikiwa Roho wa Mungu anaishi ndani yenu. Yeyote asiye na Roho wa Kristo, huyo si wake Kristo.
9Aga teie ei ela oma loomuses, vaid Vaimus, kui Jumala Vaim tõepoolest elab teie sees. Kellel ei ole aga Kristuse Vaimu, see ei ole tema oma.
10Lakini kama Kristo yumo ndani yenu, ingawa miili yenu itakufa kwa sababu ya dhambi, kwenu Roho ndiye uhai kwa sababu mmekubaliwa kuwa waadilifu.
10Kui aga Kristus on teie sees, siis on ihu küll patu tõttu surnud, aga Vaim on õiguse tõttu elu.
11Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu, basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
11Kui nüüd teis elab selle Vaim, kes Jeesuse surnuist üles äratas, siis see, kes Kristuse surnuist üles äratas, teeb ka teie surelikud ihud elavaks oma Vaimu läbi, kes teis elab.
12Hivyo basi, ndugu zangu, tunalo jukumu, lakini si la kuishi kufuatana na maumbile ya kibinadamu.
12Niisiis, vennad, et me oleme küll võlglased, kuid mitte oma loomusele, et peaksime loomuse järgi elama.
13Kwa maana, kama mkiishi kufuatana na matakwa ya maumbile ya kibinadamu, hakika mtakufa. Lakini, kama kwa njia ya Roho mnayaua matendo yenu maovu, basi, mtaishi.
13Sest kui te oma loomuse järgi elate, siis te surete; kui te aga Vaimu abil ihu teod suretate, siis te elate.
14Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
14Sest kõik, keda iganes Jumala Vaim juhib, on Jumala lapsed.
15Kwa maana, Roho mliyempokea si Roho mwenye kuwafanya ninyi watumwa na kuwatia tena hofu; sivyo, bali mmempokea Roho mwenye kuwafanya ninyi watoto wa Mungu, na kwa nguvu ya huyo Roho, sisi tunaweza kumwita Mungu, "Aba," yaani "Baba!"
15Sest te ei ole saanud orjuse vaimu, et peaksite jälle kartma, vaid te olete saanud lapseõiguse Vaimu, kelles me hüüame: 'Abba! Isa!'
16Naye Roho mwenyewe anajiunga na roho zetu na kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wa Mungu.
16Seesama Vaim tunnistab koos meie vaimuga, et me oleme Jumala lapsed.
17Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
17Kui me oleme aga lapsed, siis oleme ka pärijad, nii Jumala pärijad kui Kristuse kaaspärijad; ning kui me koos temaga kannatame, siis meid ka koos temaga kirgastatakse.
18Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyafananisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
18Sest minu arvates ei vääri nüüdse ajastu kannatused mainimist tulevase kirkuse kõrval, mida meile ilmutatakse.
19Viumbe vyote vinatazamia kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
19Sest loodu ootab pikisilmi Jumala laste ilmsikssaamist.
20Kwa maana, viumbe viliwekwa katika hali ya kutojiweza kabisa, si kwa hiari yao, ila vilifanywa hivyo kwa mapenzi ya Mungu. Hata hivyo yapo matumaini,
20Loodu on ju allutatud kaduvusele - mitte vabatahtlikult, vaid allutaja poolt -, kuid ometi lootusega,
21maana hivyo viumbe navyo vitaokolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu, vishiriki uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu.
21et ka loodu ise vabastatakse kord kaduvuse orjusest Jumala laste kirkuse vabadusse.
22Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
22Me ju teame, et kogu loodu ägab üheskoos sünnitusvaludes tänini;
23Wala si hivyo viumbe peke yake, bali hata sisi tulio na huyo Roho, aliye wa kwanza wa zawadi za Mungu; sisi pia tunalalamika ndani yetu, tukitazamia kufanywa watoto wa Mungu, nazo nafsi zenu zikombolewe.
23ent mitte üksnes loodu, vaid needki, kellel on Vaimu esmaand, ka meie ise ägame iseenestes, oodates lapseõigust, oma ihu lunastust.
24Maana kwa matumaini hayo sisi tumekombolewa; lakini tumaini halina maana ikiwa tunakiona kile tunachotumainia. Maana ni nani anayetumaini kile ambacho tayari anakiona?
24Sest me oleme päästetud lootuses. Ent juba nähtava lootmine ei ole lootus: kes siis loodab seda, mida ta näeb?
25Kama tunakitumaini kile ambacho hatujakiona bado, basi, tunakingojea kwa uvumilivu.
25Kui me aga loodame seda, mida me ei näe, siis me ootame seda kannatlikult.
26Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
26Samuti tuleb ka Vaim appi meie nõtrusele: me ju ei tea, kuidas palvetada, nõnda nagu peab, kuid Vaim ise palub meie eest sõnatute ägamistega.
27Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
27Aga südameteuurija teab, mida Vaim taotleb, sest Jumala tahtmise järgi palub ta pühade eest.
28Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi lake.
28Ent me teame, et neile, kes Jumalat armastavad, laseb Jumal kõik tulla heaks - neile, kes on tema kavatsuse kohaselt kutsutud.
29Maana hao aliowachagua tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
29Sest need, keda ta on ette ära tundnud, need ta on ka ette määranud saama tema Poja näo sarnaseks, et tema oleks esmasündinu paljude vendade seas.
30Basi, Mungu aliwaita wale aliokuwa amewateua; na hao aliowaita aliwakubali kuwa waadilifu; na hao aliowakubali kuwa waadilifu aliwashirikisha pia utukufu wake.
30Aga keda ta on ette määranud, neid on ta ka kutsunud; ja keda ta on kutsunud, need on ta ka õigeks teinud, aga keda ta on õigeks teinud, neid on ta ka kirgastanud.
31Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
31Mis me siis ütleme selle kohta? Kui Jumal on meie poolt, kes võib olla meie vastu?
32Mungu hakumhurumia hata mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
32Tema, kes oma Poegagi ei säästnud, vaid loovutas tema meie kõikide eest, kuidas ta ei peaks siis koos Pojaga meile kõike muud kinkima?
33Ni nani atakayewashtaki wateule wa Mungu? Mungu mwenyewe huwaondolea hatia!
33Kes võib süüdistada Jumala valituid? Jumal on see, kes õigeks teeb.
34Ni nani atakayewahukumu? Hakuna! Maana Kristo ndiye aliyekufa, tena alifufuka kutoka wafu na anakaa upande wa kulia wa Mungu. Yeye anatuombea!
34Kes võib meid hukka mõista? Kristus Jeesus on, kes suri ja, mis veel enam, kes üles äratati, kes on Jumala paremal käel ja kes palub meie eest.
35Ni nani awezaye kututenga na mapendo ya Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kuuawa?
35Kes võib meid lahutada Kristuse armastusest? Kas viletsus või ahistus või tagakiusamine või nälg või alastiolek või hädaoht või mõõk?
36Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha: tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa."
36Nagu on kirjutatud: 'Sinu pärast surmatakse meid kogu päeva, meid koheldakse nagu tapalambaid.'
37Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
37Kuid selles kõiges me saame täieliku võidu tema läbi, kes meid on armastanud.
38Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: wala kifo, wala uhai; wala malaika, au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka;
38Sest ma olen veendunud, et ei surm ega elu, ei inglid ega peainglid, ei praegused ega tulevased, ei väed,
39Wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.
39ei kõrgus, ei sügavus ega mis tahes muu loodu suuda meid lahutada Jumala armastusest, mis on Kristuses Jeesuses, meie Issandas.