1Tuseme nini basi? Je, twendelee kubaki katika dhambi ili neema ya Mungu iongezeke?
1Mis me siis ütleme? Kas püsida patus, et arm suureneks?
2Hata kidogo! Kuhusu dhambi sisi tumekufa--tutaendeleaje kuishi tena katika dhambi?
2Ei, mitte sugugi. Meie, kes oleme patule surnud, kuidas saaksime selles veel elada?
3Maana, mnajua kwamba sisi tuliobatizwa tukaungana na Kristo Yesu, tulibatizwa na kuungana na kifo chake.
3Kas te siis ei tea, et kes me iganes oleme Kristusesse Jeesusesse ristitud, oleme ristitud tema surmasse?
4Tulipobatizwa tuliungana na kifo chake, tukazikwa pamoja naye, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka wafu kwa kitendo kitukufu cha Baba, sisi pia tuweze kuishi maisha mapya.
4Me oleme siis koos temaga maha maetud ristimise kaudu surmasse, et otsekui Kristus on äratatud üles surnuist Isa kirkuse läbi, nõnda võime ka meie käia uues elus.
5Maana, kama sisi tumeungana naye katika kufa kama yeye, vivyo hivyo tutaungana naye kwa kufufuliwa kutoka wafu kama yeye.
5Sest kui me oleme kasvanud kokku tema surma sarnasusega, siis võime seda olla ka ülestõusmise sarnasusega,
6Tunajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja na Kristo, ili hali ya dhambi iharibiwe, tusiwe tena watumwa wa dhambi.
6teades, et meie vana loomus on koos temaga löödud risti, et see patune ihu kaotataks, nii et me kunagi enam ei orjaks pattu.
7Kwa maana, mtu aliyekufa, amenasuliwa kutoka katika nguvu ya dhambi.
7Sest kes on surnud, see on patust vabaks mõistetud.
8Basi, ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pia pamoja naye.
8Kui me oleme aga surnud koos Kristusega, siis usume, et me ka elame koos temaga,
9Maana, tunajua kwamba Kristo amekwisha fufuliwa kutoka wafu na hafi tena; kifo hakimtawali tena.
9teades, et Kristus, olles üles äratatud surnuist, enam kunagi ei sure; surm ei valitse teda enam,
10Hivyo, kwa kuwa alikufa--mara moja tu--dhambi haina nguvu tena juu yake; na sasa anaishi maisha yake katika umoja na Mungu.
10sest mis ta suri, seda ta suri patule üks kord ja alatiseks, aga mis ta elab, seda ta elab Jumalale.
11Hali kadhalika nanyi lazima mjione kuwa mmekufa kuhusu dhambi, lakini kama mnaoishi katika umoja na Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
11Nõnda arvestage ka teie endid olevat surnud patule, aga elavat Jumalale Kristuses Jeesuses.
12Kwa hiyo, dhambi isiitawale tena miili yenu ambayo hufa, na hivyo kuzitii tamaa zake.
12Ärgu siis valitsegu patt kuningana teie surelikus ihus, nii et te tema himudele oleksite kuulekad.
13Wala msitoe hata sehemu moja ya miili yenu iwe chombo cha kutenda uovu na dhambi. Badala yake, jitoleeni ninyi wenyewe kwa Mungu kama watu waliofufuliwa kutoka wafu; toeni nafsi zenu zote kwa Mungu kwa ajili ya uadilifu.
13Ärge ka loovutage oma ihuliikmeid ülekohtu relviks patule, vaid loovutage end Jumalale nagu need, kes on saanud surnuist elavaks, ja oma ihuliikmed õiguse relviks Jumalale.
14Maana, dhambi haitawatawala ninyi tena, kwani hamko chini ya Sheria, bali chini ya neema.
14Sest patt ei valitse enam teie üle, kuna te ei ole Seaduse, vaid armu all.
15Basi, tuseme nini? Je, tutende dhambi ati kwa sababu hatuko chini ya Sheria bali chini ya neema? Hata kidogo!
15Kuidas siis nüüd? Kas hakkame tegema pattu, kuna me ei ole Seaduse, vaid armu all? Kindlasti mitte!
16Mnajua kwamba mkijitolea ninyi wenyewe kama watumwa na kumtii fulani, mnakuwa kweli watumwa wake mtu huyo--au watumwa wa dhambi, na matokeo yake ni kifo, au wa utii, na matokeo yake ni kukubaliwa kuwa waadilifu.
16Eks te tea, et kelle kuulekusse teie end loovutate orjaks, kelle sõna te kuulate, selle orjad te olete - olgu patu orjad surmaks või kuulekuse orjad õiguseks!
17Ingawa mlikuwa watumwa wa dhambi zamani, sasa lakini--namshukuru Mungu--mmetii kwa moyo wote yale maazimio na mafundisho mliyopokea.
17Aga tänu Jumalale, et te olite küll patu orjad, aga nüüd olete saanud südamest kuulekaks sellele õpetusele, millesse teid on juhatatud,
18Mlikombolewa kutoka utumwa wa dhambi, mkawa watumwa wa uadilifu.
18ja patust vabastatuna olete saanud õiguse teenriteks.
19(Hapa natumia lugha ya kawaida ya watu kwa sababu ya udhaifu wenu wenyewe.) Kama vile wakati fulani mlivyojitolea ninyi wenyewe kutumikia uchafu na uhalifu kwa ajili ya uovu, vivyo hivyo sasa jitoleeni nafsi zenu wenyewe kutumikia uadilifu kwa ajili ya utakatifu.
19Ma räägin inimlikul kombel teie loomuse nõtruse pärast. Sest nii nagu te oma liikmed andsite orjaks rüvedusele ja ülekohtule, et teha ülekohut, nõnda andke nüüd oma liikmed õiguse teenritena pühitsuse jaoks.
20Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na uadilifu.
20Sest kui te olite patu orjad, siis te olite vabad õigusest.
21Sasa, mlipata faida gani siku zile kutokana na mambo yale ambayo mnayaonea aibu sasa? Maana, matokeo ya mambo haya ni kifo!
21Millist vilja te siis kandsite? Niisugust, mille pärast te nüüd häbenete. Sest selle tulemus on surm.
22Lakini sasa, mmekwisha kombolewa kutoka utumwa wa dhambi na mmekuwa watumishi wa Mungu; faida mliyo nayo sasa ni utakatifu, na matokeo yake ni uzima wa milele.
22Nüüd aga, kui te olete vabastatud patust ja saanud Jumala teenriteks, te kannate vilja pühitsuseks. Ja selle tulemus on igavene elu.
23Kwa maana mshahara wa dhambi ni kifo; lakini zawadi anayotoa Mungu ni uzima wa milele katika kuungana na Kristo Yesu, Bwana wetu.
23Sest patu palk on surm, aga Jumala armuand on igavene elu Kristuses Jeesuses, meie Issandas.