Swahili: New Testament

Estonian

Titus

1

1Mimi Paulo, mtumishi wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo naandika. Mimi nimechaguliwa kuijenga imani ya wateule wa Mungu na kuwaongoza waufahamu ukweli wa dini yetu,
1Paulus, Jumala sulane ning Jeesuse Kristuse apostel Jumalast valitute usu järgi ja selle tõe tunnetuse järgi, mis vastab jumalakartusele,
2ambayo msingi wake ni tumaini la kupata uzima wa milele. Mungu ambaye hasemi uongo, alituahidia uzima huo kabla ya mwanzo wa nyakati,
2igavese elu lootuse põhjal, mille Jumal, kes ei valeta, on tõotanud enne igavesi aegu,
3na wakati ufaao ulipowadia, akaudhihirisha katika ujumbe wake. Mimi nilikabidhiwa ujumbe huo nuutangaze kufuatana na amri ya Mungu, Mwokozi wetu.
3ja kes on määratud ajal teinud oma sõna avalikuks jutlustamise läbi, mis on usaldatud minu kätte Jumala, meie Päästja käsu kohaselt, -
4Ninakuandikia wewe Tito, mwanangu wa kweli katika imani tunayoshiriki. Nakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba, na kutoka kwa Kristo Yesu, Mkombozi wetu.
4Tiitusele, tõelisele pojale meie ühise usu poolest: Armu ja rahu Jumalalt Isalt ja Issandalt Jeesuselt Kristuselt, meie Päästjalt!
5Nilikuacha Krete ili urekebishe yale mambo ambayo hayakuwa yamekamilika bado, na kuwateua wazee wa kanisa katika kila mji. Kumbuka maagizo yangu:
5Ma jätsin su Kreetale maha selleks, et sa seaksid korda, mis jäi korraldamata, ning seaksid vanemaid igasse linna, nagu ma tegin sulle ülesandeks:
6mzee wa kanisa anapaswa kuwa mtu asiye na hatia; aliye na mke mmoja tu, na watoto wake wanapaswa kuwa waumini, wasiojulikana kuwa wakorofi au wakaidi.
6kui keegi on laitmatu - ühenaisemees, kellel on usklikud lapsed, keda ei süüdistata ulaelus ega allumatuses.
7Maana kwa vile kiongozi wa kanisa ni mkurugenzi wa kazi ya Mungu, anapaswa kuwa mtu asiye na hatia. Asiwe mwenye majivuno, mwepesi wa hasira, mlevi, mkorofi au mchoyo.
7Sest ülevaataja peab Jumala majapidajana olema laitmatu: selline, kes ei ole ennast täis, äkiline, joomar, kakleja, liigkasuvõtja,
8Anapaswa kuwa mkarimu na anayependa mambo mema. Anapaswa kuwa mtu mtaratibu, mwadilifu, mtakatifu na mwenye nidhamu.
8vaid külalislahke, head armastav, mõõdukas, õiglane, vaga, kasin,
9Ni lazima ashike kikamilifu ujumbe ule wa kuaminika kama unavyofundishwa. Ndivyo atakavyoweza kuwatia wengine moyo kwa mafundisho ya kweli na kuyafichua makosa ya wale wanaoyapinga mafundisho hayo.
9kes peab kinni õpetusekohasest ustavast sõnast, nii et ta oleks suuteline niihästi manitsema terve õpetuse varal kui ka ümber veenma vasturääkijaid.
10Maana, wako watu wengi, hasa wale walioongoka kutoka dini ya Kiyahudi, ambao ni wakaidi, wanaowapotosha wengine kwa upumbavu wao.
10Sest on palju vastuhakkajaid, lobisejaid ja eksitajaid, eriti ümberlõigatute seas,
11Lazima kukomesha maneno yao, kwani wanavuruga jumuiya nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi kufundisha; wanafanya hivyo kwa nia mbaya ya kupata faida ya fedha.
11kelle suu tuleb sulgeda, sest nad pööravad ära terved pered, õpetades häbiväärsest kasuhimust seda, mida ei peaks.
12Hata mmoja wa manabii wao, ambaye naye pia ni Mkrete, alisema: "Wakrete, husema uongo daima; ni kama wanyama wabaya, walafi na wavivu!"
12Üks nende seast, nende oma prohvet, on öelnud: 'Kreetalased on luiskajad, tigedad loomad, laisklejad vatsad.'
13Naye alitoboa ukweli kwa sababu hiyo, unapaswa kuwakaripia vikali, ili wawe na imani kamilifu.
13See tunnistus on tõsi. Sel põhjusel noomi neid karmilt, et nad oleksid usult terved,
14Wasiendelee kushikilia hadithi tupu za Kiyahudi na maagizo ya kibinadamu yanayozuka kwa watu walioukataa ukweli.
14ei hooliks juudi müütidest ega tõele selja pööranud inimeste käskudest.
15Kila kitu ni safi kwa watu walio safi; lakini hakuna chochote kilicho safi kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, maana dhamiri na akili zao zimechafuliwa.
15Puhtaile on kõik puhas, aga rüvedaile ja uskmatuile pole miski puhas, vaid rüve on nii nende meel kui südametunnistus.
16Watu kama hao hujidai kwamba wanamjua Mungu, lakini kwa matendo yao humkana. Ni watu wa kuchukiza mno na wakaidi, hawafai kwa jambo lolote jema.
16Nad väidavad end tundvat Jumalat, aga tegudega salgavad tema, sest nad on jäledad ja sõnakuulmatud ega ole ühelegi heale teole kõlblikud.