Swahili: New Testament

Paite

Matthew

5

1Yesu alipoyaona makundi ya watu, alipanda mlimani, akaketi. Wanafunzi wake wakamwendea,
1Huchiin, mipite tuh a muhin tangah a pai tou a, huan, a tu a, a nungjuite a kiangah a hongpai ua; huan thu a gen a,
2naye akaanza kuwafundisha:
2amau thu a hilh a:
3"Heri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
3Lungsima gentheite a hampha uh vangam amaua ahi ngala.
4Heri walio na huzuni, maana watafarijiwa.
4Lungkhamte a hampha uh; khamuan a om ding ahi ngal ua
5Heri walio wapole, maana watairithi nchi.
5Thunuailutte a hampha uh; lei gou luah ding ahi ngal ua.
6Heri wenye njaa na kiu ya kufanya atakavyo Mungu, maana watashibishwa.
6Diktatna lunggulha gilkiala dangtak te a hampha uh; tai ding ahi ngal ua.
7Heri walio na huruma, maana watahurumiwa.
7Zahngai theite a hampha uh; zahngaihna mu ding ahi ngal ua.
8Heri wenye moyo safi, maana watamwona Mungu.
8Lungsima siangthoute a hampha uh; Pathian mu ding ahi ngal ua.
9Heri wenye kuleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu.
9Lemna bawlte a hampha uh; Pathian tate chih ding ahi ngal ua.
10Heri wanaoteswa kwa sababu ya kufanya atakavyo Mungu, maana ufalme wa mbinguni ni wao.
10Diktakna jiak a sawina thuakte a hampha uh, vangam amaua ahi ngal a.
11"Heri yenu ninyi watu wakiwatukana, wakiwadhulumu na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa ajili yangu.
11Min keima jiaka hontai ua, a hon sawi ua, juaua gilou chitenga a honhek hun chiangun, na hampha uh.
12Furahini na kushangilia maana tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Hivyo ndivyo walivyowadhulumu manabii waliokuwako kabla yenu.
12Kipak unla, nakpitakin nuam un; van ah na kipahman uh a thupi ngala: tuamah bangin na ma ua jawlnei omte leng a nasawi nak uhi.
13"Ninyi ni chumvi ya dunia! Lakini chumvi ikipoteza ladha yake itakolezwa na nini? Haifai kitu tena, ila hutupwa nje na kukanyagwa na watu.
13Lei chi na hi uh: himahleh chi peng leh, bangin ahia a kihih-al nawn ding? Paihkhiaka mihingte chil gawpgawp lou ngal dingin, bangmah din a phatuam kei.
14"Ninyi ni mwanga wa ulimwengu! Mji uliojengwa juu ya mlima hauwezi kufichika.
14Khovel vakna na hi uh. Tang tunga kho om selguk theih ahi kei.
15Wala watu hawawashi taa na kuifunika kwa chungu, ila huiweka juu ya kinara ili iwaangazie wote waliomo nyumbani.
15Min khawnvak dein loh nuai ah a koih ngei kei uh. a koihna ah a koih jaw uh. Huchiin in sunga mi om tengteng atan hi
16Vivyo hivyo, ni lazima mwanga wenu uangaze mbele ya watu, ili wayaone matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni."
16Huchimah bangin, na vak uh mi mit muh dingin vak hen, huchiin na thilhih hoihte uh a mu ding ua, na Pa uh vana om a pahtawi thei ding uh.
17"Msidhani ya kuwa nimekuja kutangua Sheria ya Mose na mafundisho ya manabii. Sikuja kutangua bali kukamilisha.
17Dan thu hiam, jawlneite thu hiam hihmang dinga hongpai ka hih um kei un; hihmang dinga hongpai ka hi kei, hih tangtung dinga hongpai ka hi jaw.
18Kweli nawaambieni, mpaka hapo mbingu na dunia zitakapopita, hakuna hata nukta moja au sehemu ndogo kabisa ya Sheria itakayoondolewa, mpaka yote yametimia.
18Chih taktakin ka honhilh ahi, lei leh van a man masiah dan thua sut vom neu chik hiam, thai vom neu chik hiam, khat leng a mang keihial ding, a veka atun kim masiah uh.
19Basi, yeyote atakayevunja hata amri moja ndogo kuliko zote, na kuwafundisha wengine wafanye hivyo, huyo atakuwa mdogo kabisa katika Ufalme wa mbiguni. Lakini yule atakayezishika na kuwafundisha wengine, huyo atakuwa mkubwa katika Ufalme wa mbinguni.
19Huchiin, kuapeuh hiai thupiak neupente laka a khat lel leng jui lou a, tuabanga hih dia mite thuhilh peuhmah, vangamah mi neupen a kichi ding hi; ahihhangin, kuapeuhmah juia thuhilh behlap tuh, vangamah mi lian a kichi ding hi.
20Ndiyo maana nawaambieni, wema wenu usipozidi ule wa Mafarisayo na walimu wa Sheria, hamtaingia kamwe katika Ufalme wa mbinguni.
20Na diktatna un laigelhmite leh Pharisaite diktatna a khup ken jaw vangamah na lut kei hial ding uh chih ka honhilh ahi.
21"Mmekwisha sikia ya kuwa watu wa kale waliambiwa: Usiue! Atakayeua lazima ahukumiwe.
21Nidang laia mite kianga, Tual na that ding ahi kei, kichi leh, kuapeuh tualthat tuh vaihawmnaa din lauhthawnhuai takin a om ding uh, ki chi na zata uh;
22Lakini mimi nawaambieni, yeyote anayemkasirikia ndugu yake, lazima ahukumiwe. Anayemdharau ndugu yake atapelekwa mahakamani. Anayemwita ndugu yake: Pumbavu atastahili kuingia katika moto wa Jehanamu.
22Ken jaw, Kuapeuh a unau tunga heh tuh vaihawmnaa din lauhthawnhuai tak in a om ding; huan kuapeuh a unau selphou tuh vaihawmmite hawmsaka om lauthawnhuai takin a om ding; huan, kuapeuh, Nang mihai chi tuh, Gehenna meia paih lauhthawnhuai takin a om ding uh chih ka honhilh ahi.
23Basi, ukipeleka sadaka yako mbele ya madhabahu na hapo ukakumbuka kwamba ndugu yako ana ugomvi nawe,
23Huai jiakin, maitam bula na thilpiak na lat lel laia na unauin na tungah lunghihlouhna a nei chih na thei khiak leh.
24iache sadaka yako mbele ya madhabahu, nenda kwanza ukapatane na ndugu yako, ndipo urudi ukatoe sadaka yako.
24Huai maitam ma ah na thilpiak tuh nusia inla, pai inla na unau kilempih phot inla huan na thilpiak lan in.
25"Patana na mshtaki wako upesi mkiwa bado njiani, kwenda mahakamani. La sivyo, mshtaki wako atakukabidhi kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa askari, nawe utafungwa gerezani.
25Na langpa tuh vaihawmnain juana lampia na pai khawm lai un lem zok in, huchilou in jaw na langpan thukhenmi khut ah honpe dia, thukhenmin mimanpa kiangah a honpe dia; suangkulh ah a honkhum kha ding uh.
26Kweli nakwambia, hutatoka humo mpaka umemaliza kulipa senti ya mwisho.
26chihtaktakin ka hon hilh ahi, Paihsasan khat nangawn na piak kim masiah huailaia kipanin na pawt khe kei hilhial ding.
27"Mmesikia ya kuwa watu waliambiwa: Usizini!
27Ang na kawm ding ahi kei, kichi na jata uh. Ken jaw,
28Lakini mimi nawaambieni, atakayemtazama mwanamke kwa kumtamani, amekwisha zini naye moyoni mwake.
28Kuapeuh numei khelhpih utna toh en tuh, a lungsimin ang a kawm khinta chih ka hinhilh ahi.
29Basi, kama jicho lako la kulia linakukosesha, ling'oe ukalitupe mbali. Afadhali zaidi kwako kupoteza kiungo kimoja cha mwili wako, kuliko mwili wako wote kutupwa katika moto wa Jehanamu.
29Huan, na mit taklamin a honhihpuk leh, khel khia inla, pai mai in, na sapumpi a puma Gehenna a pai sangin na sapuma ka khat manthat nanga dingin a hoih hi.
30Na kama mkono wako wa kulia unakukosesha, ukate ukautupe mbali. Afadhali zaidi kupoteza kiungo kimoja cha mwili, kuliko mwili wako wote uende katika moto wa Jehanamu.
30Huan, na khut taklamin a honhihpuk leh, tan inla, pai mai in; na sapumpi a puma Genhenna a pai sangin, na sapum a ka khat manthat nanga dingin a hoih jaw hi.
31"Ilikwisha semwa pia: Anayemwacha mke wake, yampasa ampe hati ya talaka.
31Kuapeuh zi main kimakna lai a kiangah pia heh, leng a kichi.
32Lakini mimi nawaambieni, anayempa mkewe talaka, isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, anamfanya azini; na mtu akimwoa mwanamke aliyepewa talaka, anazini.
32Ken jaw kuapeuh tangval ngaih jiak hi lou a, zi main amah tuh angkawmsak ahi, huan, kuapeuh maksa nung nei tuh angkawm ahi chih ka honhilh ahi.
33"Tena mmesikia kuwa watu wa kale waliambiwa: Usivunje kiapo chako, bali ni lazima utimize kiapo chako kwa Bwana.
33Nidanglaiin mite kiangah, Juauin kichiam kenla, Toupa kiangah na kichiam nate tuh tangtun jawin, a kichi chih leng na zata uh.
34Lakini mimi nawaambieni, msiape kamwe; wala kwa mbingu, maana ni kiti cha enzi cha Mungu;
34Ken jaw, ka honhilh ahi, Chiam himhim kichiam kei un; van louin kichiam kei un, huai tuh Pathian laltutphah ahi ngala; lei louin kichiam sam kei un, huai tuh a khe ngakna ahi ngal a.
35wala kwa dunia, maana ni kiti chake cha kuwekea miguu; wala kwa Yerusalemu, maana ni mji wa Mfalme mkuu.
35Jerusalem louin kichiam sam kei un, huai tuh Kumpipa thupitak khopi ahi ngala.
36Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kuufanya hata unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.
36Na lu louin na kichiam ding ahi sam kei, sam zang khat leng na hihngouin, na hihdum thei ngal kei a.
37Ukisema, Ndiyo, basi iwe Ndiyo; ukisema Siyo, basi iwe kweli Siyo. Chochote kinachozidi hayo hutoka kwa yule Mwovu.
37Na thugen uh, A hi, ahi. Hi lou, hilou, hi vanglak heh; a kan a val jaw gitlouhna laka suak ahi.
38"Mmesikia kwamba ilisemwa: Jicho kwa jicho, jino kwa jino.
38Mit sikin mit, ha sikin ha a kichi chih na zata uh.
39Lakini mimi nawaambieni, usimlipize kisasi mtu mbaya. Mtu akikupiga kofi shavu la kulia, mgeuzie pia shavu la pili.
39Ken jaw ka honhilh ahi. Mi gilou nang kei un; na biang taklam bengte tuh, a lehlam leng doh jaw un.
40Mtu akikupeleka mahakamani kutaka kukuchukulia shati lako, mwache achukue pia koti lako.
40Huan kuapeuhin na lakah thusia bawlin, na puannak lak a tup leh, na puanja leng lasak ngal in.
41Mtu akikulazimisha kubeba mzigo wake kilomita moja, ubebe kilomita mbili.
41Huan mel khat pai dia honphut teitei kiangah mel nih paisak in.
42Akuombaye mpe, na mtu akitaka kukukopa kitu usimnyime.
42A honngen kiangah pia inla, na laka leitawi nuam tuh kiheisan ken.
43"Mmesikia kwamba ilisemwa: Mpende jirani yako na kumchukia adui yako.
43Na vengte it inla, na melmate hua in, a kichi chih na zata uh.
44Lakini mimi nawaambieni, wapendeni adui zenu na kuwaombea wale wanaowadhulumu ninyi
44Ken jaw ka honhilh ahi, na melmate uh it unla, a honsawite thum sak un;
45ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaangazia jua lake watu wabaya na wema, na kuwanyeshea mvua watu wanyofu na waovu.
45na Pa uh vana om tate na hih theihna ding un, aman tuh migiloute leh mi hoihte tungah a ni a suak saka, mi diktatte leh diktatloute tungah leng vuah a zu sak.
46Je, mtapata tuzo gani kwa kuwapenda tu wale wanaowapenda ninyi? Hakuna! Kwa maana hata watoza ushuru hufanya hivyo!
46Nou honitte kia na it un, kipahman bang ahia na muh ding un? siahkhonmiten leng huchihbangin a hihsam kei ua ahia?
47Kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, je, mmefanya kitu kisicho cha kawaida? Hata watu wasiomjua Mungu nao hufanya vivyo hivyo.
47Huan, na unaute kia uh chibai na buk un bang na hih tam tuan ua ahia? Jentelten leng hichi bangin a hih sam kei ua hia?Huchiin, na Pa uh vana om a hoih kim sipsip bangin na hoih kim sipsip ding uh ahi.
48Basi, muwe wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
48Huchiin, na Pa uh vana om a hoih kim sipsip bangin na hoih kim sipsip ding uh ahi.