1Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
1Huan longah a luta, a galkaha, amah khua a hongtungta hi.
2Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako."
2Huan, ngaiin, mi khat zenga damlou, lupnaa lum a hon jawng ua; huchiin, Jesun a ginna uh muin, zenga damloupa kiangah, Tapa, khamuangin om in, na khelhnate ngaihdam hihen, a chi a.
3Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, "Mtu huyu anamkufuru Mungu!"
3Huan, ngaiin, laigelhmi kuatehiam a kingaihtuah ua, Hiai miin Pathian a gensia, chiin.
4Yesu aliyajua mawazo yao, akasema, "Kwa nini mnawaza mabaya mioyoni mwenu?
4Huchiin Jesun a ngaihtuahte uh a thei a, bangdia na lung ua gilou ngaihtuah na hi ua? a chi a.
5Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Simama, utembee?
5Na khelhnate ngaihdam hihen, chih leh, Thou inla, khein pai in, chih a koi a baihlam zaw
6Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Inuka, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako."
6Himahleh Mihing Tapain leitung ah khelhnate ngaih dam theihna a nei chih na theihna ding un, (zenga damloupa kiangah) Thouin, na lupna la inla, na inah pai in, achia.
7Huyo mtu aliyekuwa amepooza akainuka, akaenda nyumbani kwake.
7Huchiin a thoua, a in ah a paita hi.
8Watu wote katika ule umati walipoona hayo, walishangaa na kuogopa; wakamtukuza Mungu aliyewapa binadamu uwezo wa namna hiyo.
8A hihhangin mipiin a muh un, lamdang a sa ua huchibang hihtheihna mihingte kianga pepa, Pathian a pahtawita uhi.
9Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda zake, alimwona mtu mmoja aitwaye Mathayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Basi, Yesu akamwambia, "Nifuate." Naye Mathayo akainuka, akamfuata.
9HUan, Jesu huai a kipanin a pai jela, siahpiakna mun a tu, mi khat, amin Matthai a mu a; huan, a kiangah, Honjui in, a chi a. Huchiin, a thou a, a juita.
10Yesu alipokuwa nyumbani ameketi kula chakula, watoza ushuru wengi na wahalifu walikuja wakaketi pamoja naye na wanafunzi wake.
10Huan, hichi ahia, ina ankuang a um laiin, ngaiin, siahkhonmite leh mikhialte tampi a hongpai ua, Jesu leh a nungjuite tuh a umpih chiat ua.
11Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi wake, "Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
11Huan Pharisaiten huai a muh un, a nungjuite kiangah, bangdia na heutupa un siahkhonmite leh mikhialte kianga ne ahia? a chi ua.
12Yesu aliwasikia, akasema, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi.
12Himahleh, Jesun huai a jak takin, Mi hatten daktor a kiphamoh kei ua, mi damtheilouten a kiphamoh jaw uh.
13Basi, kajifunzeni maana ya maneno haya: Nataka huruma, wala si dhabihu. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi."
13Huchiin, Kithoihna deihlou in zahngaihna ka deih hi, chih, a omdan vazil un, mi diktatte sam dia hongpai k ahi kei, mikhialte sam dia hongpai ka hizaw, achia.
14Kisha wanafunzi wa Yohane mbatizaji walimwendea Yesu, wakamwuliza, "Sisi na Mafarisayo hufunga mara nyingi; mbona wanafunzi wako hawafungi?"
14Huchih laiin Johan nungjuite a kiangah a hongpai ua, Bangdia kou leh Pharisaiten an ngawl gige a, na nungjuiten ngawl lou uh ahia? a chi ua.
15Yesu akawajibu, "Je, walioalikwa arusini wanaweza kuomboleza wakati bwana arusi yupo pamoja nao? La hasha! Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
15Huan, Jesun a kianguah, Mou pite kianga a pasal ding a omlai teng mou piten a sun thei ua hia? Himahleh, a pasal ding tuh a kiang ua kipana pi mang nite a hongtung dinga, huai hun chiangin an a honngawl ding uh.
16"Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu. Maana kiraka hicho kitararua hilo vazi kuukuu, na pale palipokuwa pameraruka pataongezeka.
16Huan, kuamahin puan lui puan tuikhai louh themin a thuap ngei kei uh; a thuapna dingin puan tuh a kaikek zo ding, a hong nakkek zo sem ding.
17Wala hakuna mtu awekaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, viriba hupasuka na divai ikamwagika, navyo viriba vikaharibika. Ila divai mpya hutiwa katika viriba vipya, na vyote viwili, viriba na divai, vikahifadhiwa salama."
17Kuamahin uain thak savun uain-thawl luiah a thun ngei kei uh; huchilou injaw savun thawlte a puak kek dia, uain, tuh a bo dia, savun-thawl leng a hongse ding; huaijiakin uain thak tuh savun uainthawl thakah a thun jaw ua, huchiin hoihtakin a om tuaktuak, a chi a.
18Yesu alipokuwa akisema hayo, ofisa mmoja Myahudi alifika, akamwinamia na kusema, "Binti yangu amekufa sasa hivi. Lakini, tafadhali njoo umwekee mkono wako naye ataishi."
18Huan a kiang ua a gen laitakin, ngaiin, vaihawmpa khat a hongpaia, chibai a buka, Ka tanu tu takin a si a; himahleh, hongpai inla, a tungah na khut koih lechin, honghing nawn ding, achia.
19Yesu akaondoka pamoja na wanafunzi wake, akamfuata.
19Huchiin, Jesu a thoua, a juita a, nungjuiten leng a jui sam uh.
20Mama mmoja, mgonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake.
20Huan, ngaiin, numei khat, kum sawm leh kum nih si pawta damlou, a nungah a hongpai a, a puan mong a khoiha;
21Alifanya hivyo kwani alifikiri moyoni: "Nikigusa tu vazi lake, nitapona."
21A puan mongkia khoih lengleng, hihdamin ka om mai ding, a lungsimin a chi a.
22Basi, Yesu akageuka akamwona, akamwambia, "Binti, jipe moyo! Imani yako imekuponya." Mama huyo akapona saa ileile.
22Huan, Jesu a kihei a, amah a mu a, Ka tanu, khamuang takin om in; na ginna na dampih hi, a chi a. Huchiin, numeinu tuh huaidak a kipan a hongdamta.
23Kisha Yesu akaingia nyumbani kwa yule ofisa. Na alipowaona wapiga filimbi na umati wa watu wanaofanya matanga,
23Huan, Jesu vaihawmpa in ah a luta, tamngai tumte leh mipi thawmngaih vengvungte a va muhin.
24akasema, "Ondokeni hapa! Msichana huyu hakufa, amelala tu." Nao wakamcheka.
24Pawt un: naupang a si kei, a ihmu ahi jaw, achi a. Huan, amau tuh amah a nuihsan maimah ua.
25Basi, umati wa watu ulipoondolewa, Yesu aliingia ndani, akamshika huyo msichana mkono, naye akasimama.
25Himahleh, mipi tuh delh khiaka a om nung un, alut a, a khut ah a len a, naupang tuh a hongthouta a.
26Habari hiyo ikavuma sana katika nchi ile yote.
26Huan, huai tanchin tuh huai gam tengteng ah a hongthang kheta.
27Yesu aliondoka hapo, na alipokuwa anakwenda, vipofu wawili walimfuata wakipiga kelele, "Mwana wa Daudi, utuhurumie!"
27Huan, Jesu huai a kipanin a pai jela, mittaw nihin, David Tapa, ka tunguah zahngai in, chia, kikou in a jui ua.
28Yesu alipoingia nyumbani, vipofu hao wawili wakamwendea, naye akawauliza, "Je, mnaamini kwamba naweza kuwafanyia jambo hilo?" Nao wakamjibu, "Naam, Mheshimiwa."
28Huan, in a a lut leh, mittawte tuh a kiangah a hongpai ua; huan, Jesun a kiang uah. Hiai hih theiin na hongingta uh hia? a chi a. Amau tuh a kiangah, Gingta e, Toupa, a chi ua.
29Hapo Yesu akayagusa macho yao, akasema, "Na iwe kwenu kama mnavyoamini."
29Huan, aman tuh a mit uh a khoiha, Na gintak bang un na tunguah tung heh, a chi a. Huchiin, a mit uh a hong vakta a.
30Macho yao yakafunguliwa. Naye Yesu akawaonya kwa ukali: "Msimwambie mtu yeyote jambo hili."
30Huan, Jesun a kianguah, Kuamah theih louh dingin pilvang un, achi bilbela.
31Lakini wao wakaondoka, wakaeneza habari za Yesu katika nchi ile yote.
31Himahleh, amau tuh a pawt ua, huai gam tengteng ah a tanchin a hihthangta uh.
32Watu walipokuwa wanakwenda zao, wengine walimletea Yesu mtu mmoja aliyekuwa bubu kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo.
32Huan, a pawt laitak un, ngaiin, dawi mat pautheilou khat a kiangah a honpi ua.
33Mara tu huyo pepo alipotolewa, mtu huyo aliyekuwa bubu akaanza kuongea tena. Watu wakashangaa na kusema, "Jambo kama hili halijapata kuonekana katika Israeli!"
33Huan, dawi tuh a delh khiak takin pautheilou tuh a hongpauta a; Huan mipiten lamdang a sa mahmah ua, Israelte lakah hichibang a mu ngei kei uh, a chi ua.
34Lakini Mafarisayo wakawa wanasema, "Anawatoa pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo wabaya."
34Pharisaiten bel, Dawi lal vangin ahi, dawite a delh khiak nak, a chi ua.
35Yesu alitembelea miji yote na vijiji, akafundisha katika masunagogi yao akihubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila namna.
35Huan, Jesun a kikhopnain khawng ua hilhin, Gam Tanchin Hoih tuh genin, dam louhna chiteng leh natna chiteng khawng hihdamin, kho lian leh kho neu tengteng a tawn vialviala.
36Basi, alipowaona watu, makundi kwa makundi, aliwaonea huruma kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.
36Huchiin, mipiten a muhin, chingding neilou belamte banga gimthuak leh dalha a om jiak un a hehpihta mahmah a,
37Hapo akawaambia wanafunzi wake, "Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache.
37Huchiin, a nungjuite kiangah, Buh lak dinglah a tam mahmaha, himahleh, a semmite a tawm uh;huaijiakin a buh la ding a semdingte sawl dingin buh Neipa kiangah ngen un, a chi a.
38Kwa hivyo mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake."
38huaijiakin a buh la ding a semdingte sawl dingin buh Neipa kiangah ngen un, a chi a.