World English Bible

Swahili: New Testament

Luke

2

1Now it happened in those days, that a decree went out from Caesar Augustus that all the world should be enrolled.
1Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
2This was the first enrollment made when Quirinius was governor of Syria.
2Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
3All went to enroll themselves, everyone to his own city.
3Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
4Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, into Judea, to the city of David, which is called Bethlehem, because he was of the house and family of David;
4Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
5to enroll himself with Mary, who was pledged to be married to him as wife, being pregnant.
5Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
6It happened, while they were there, that the day had come that she should give birth.
6Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
7She brought forth her firstborn son, and she wrapped him in bands of cloth, and laid him in a feeding trough, because there was no room for them in the inn.
7akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
8There were shepherds in the same country staying in the field, and keeping watch by night over their flock.
8Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
9Behold, an angel of the Lord stood by them, and the glory of the Lord shone around them, and they were terrified.
9Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
10The angel said to them, “Don’t be afraid, for behold, I bring you good news of great joy which will be to all the people.
10Malaika akawaambia, "Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
11For there is born to you, this day, in the city of David, a Savior, who is Christ the Lord.
11Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
12This is the sign to you: you will find a baby wrapped in strips of cloth, lying in a feeding trough.”
12Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini."
13Suddenly, there was with the angel a multitude of the heavenly army praising God, and saying,
13Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
14“Glory to God in the highest, on earth peace, good will toward men.”
14"Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!"
15It happened, when the angels went away from them into the sky, that the shepherds said one to another, “Let’s go to Bethlehem, now, and see this thing that has happened, which the Lord has made known to us.”
15Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: "Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha."
16They came with haste, and found both Mary and Joseph, and the baby was lying in the feeding trough.
16Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
17When they saw it, they publicized widely the saying which was spoken to them about this child.
17Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
18All who heard it wondered at the things which were spoken to them by the shepherds.
18Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
19But Mary kept all these sayings, pondering them in her heart.
19Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
20The shepherds returned, glorifying and praising God for all the things that they had heard and seen, just as it was told them.
20Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
21When eight days were fulfilled for the circumcision of the child, his name was called Jesus, which was given by the angel before he was conceived in the womb.
21Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
22When the days of their purification according to the law of Moses were fulfilled, they brought him up to Jerusalem, to present him to the Lord
22Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
23(as it is written in the law of the Lord, “Every male who opens the womb shall be called holy to the Lord”),
23Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: "Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana."
24and to offer a sacrifice according to that which is said in the law of the Lord, “A pair of turtledoves, or two young pigeons.”
24Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
25Behold, there was a man in Jerusalem whose name was Simeon. This man was righteous and devout, looking for the consolation of Israel, and the Holy Spirit was on him.
25Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
26It had been revealed to him by the Holy Spirit that he should not see death before he had seen the Lord’s Christ.
26Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
27He came in the Spirit into the temple. When the parents brought in the child, Jesus, that they might do concerning him according to the custom of the law,
27Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
28then he received him into his arms, and blessed God, and said,
28Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
29“Now you are releasing your servant, Master, according to your word, in peace;
29"Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30for my eyes have seen your salvation,
30Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
31which you have prepared before the face of all peoples;
31ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
32a light for revelation to the nations, and the glory of your people Israel.”
32Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli."
33Joseph and his mother were marveling at the things which were spoken concerning him,
33Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
34and Simeon blessed them, and said to Mary, his mother, “Behold, this child is set for the falling and the rising of many in Israel, and for a sign which is spoken against.
34Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, "Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
35Yes, a sword will pierce through your own soul, that the thoughts of many hearts may be revealed.”
35na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako."
36There was one Anna, a prophetess, the daughter of Phanuel, of the tribe of Asher (she was of a great age, having lived with a husband seven years from her virginity,
36Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
37and she had been a widow for about eighty-four years), who didn’t depart from the temple, worshipping with fastings and petitions night and day.
37Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
38Coming up at that very hour, she gave thanks to the Lord, and spoke of him to all those who were looking for redemption in Jerusalem.
38Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
39When they had accomplished all things that were according to the law of the Lord, they returned into Galilee, to their own city, Nazareth.
39Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
40The child was growing, and was becoming strong in spirit, being filled with wisdom, and the grace of God was upon him.
40Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
41His parents went every year to Jerusalem at the feast of the Passover.
41Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
42When he was twelve years old, they went up to Jerusalem according to the custom of the feast,
42Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43and when they had fulfilled the days, as they were returning, the boy Jesus stayed behind in Jerusalem. Joseph and his mother didn’t know it,
43Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
44but supposing him to be in the company, they went a day’s journey, and they looked for him among their relatives and acquaintances.
44Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
45When they didn’t find him, they returned to Jerusalem, looking for him.
45Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
46It happened after three days they found him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both listening to them, and asking them questions.
46Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47All who heard him were amazed at his understanding and his answers.
47Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
48When they saw him, they were astonished, and his mother said to him, “Son, why have you treated us this way? Behold, your father and I were anxiously looking for you.”
48Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, "Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni."
49He said to them, “Why were you looking for me? Didn’t you know that I must be in my Father’s house?”
49Yeye akawajibu, "Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?"
50They didn’t understand the saying which he spoke to them.
50Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
51And he went down with them, and came to Nazareth. He was subject to them, and his mother kept all these sayings in her heart.
51Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
52And Jesus increased in wisdom and stature, and in favor with God and men.
52Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.